0
Your Cart
No products in the cart.

Hadithi yetu

Sisi ni nani
KUHUSU AFRICA NATURE ORGANIZATION

Sisi ni nani

Haja ya kuwa na shirika la kuhamasisha jamii mashinani ili kuchangia kikamilifu katika usimamizi undelevu wa mali asili kote barani Afrika ni wazo lililo chipuza katika mjadala wa wanamazingira walio kongamana 2010 mjini Arusha, Tanzania. Lengo letu limekuwa kukuza mbinu bora za usimamizi wa mazingira na maliasili miongoni mwa jamii mashinani, kufanya kazi kwa karibu na mashirika yasiyo ya kiserikali, sekta binafsi na Serikali.

Maono Yetu

Mazingira na mali asili inayo simamiwa vyema kwa manufaa ya Watu na Wanyama Pori.

Kazi Yetu

Kuimarisha usimamizi endelevu wa mazingira na maliasili kwa kuwezesha jamii mashinani, kusaidia kujenga mifumo bora ya usimamizi wa maliasili, kukuza ubunifu endelevu wa mazingira na kuendeleza desturi za matumizi endelevu.
Huwezi kulinda mazingira kikamilifu kabla ya kujenga uwezo wa jamii, kuwapasha, na kuwasaidia kuelewa kuwa rasilimali hizi ni zao na wanahitaji kuzilinda
Professor Wangari Maathai
Profesa Wangari Maathai.

Utawala

Bodi ya shirika la Africa Nature Organization ina simamiwa na wanachama 5 wenye uzoefu mkubwa katika nyanja za mazingira, usimamizi wa maliasili, ukuzaji wa vipawa, utetezi wa sera na utafiti.

Maadili ya Msingi

Africa Nature Organization inaongozwa na maadili muhimu yafuatayo katika utendakazi wake:

Usawa na Uadilifu: Watu wote wana haki ya kupata mgao wa manufaa ya mazingira na maliasili zetu. Sambamba na hili, uzalishaji na usambazaji wa faida za rasilimali unapaswa kufanywa kwa namna ambayo itaboresha maadili na manufaa ya mazingira na maliasili na kwa kutambua usawa na haki ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Matumizi endelevu: Tuna amini matumizi endelevu ya mazingira na maliasili kutawezesha kuwepo kwa huduma muhimu za ki-ikolojia kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Ushirikiano: Tuna tambua kazi kubwa iliyoko ya kujenga mifumo endelevu ya usimamizi wa mazingira na maliasili. Katika kutekeleza jukumu letu, tutafanya kazi kwa karibu na kwa ushirikiano na jamii mashinani, mashirika yasiyo ya Serikali, mashirika ya kibinafsi na Serikali ili kutekeleza majukumu yetu ipasavyo.

Utaalamu: Tumejitolea kuafikia Maono yetu kwa kutekeleza vyema kazi yetu. Tutatekeleza kazi yetu kwa bidii na kwa kuzingatia viwango vya juu vya maadili na utaalamu vinavyotambulika kitaifa na kimataifa.

Unyumbufu: Tunafanya kazi katika mazingira yanayobadilika mara kwa mara na ambayo yanahitaji wepesi wa mabadiliko ya mikakati na zana zetu kulingana na mahitaji.

Want to be a part of our initiative?

Our testimonials

What they’re talking about our policy

Lorem Ipsum is simply dummy text of free available in market the printing and typesetting industry has been.
Team members

Meet our best professional insurance agents

swSwahili